Friday, November 15, 2013
MSEVENI NAE AMTOSA RAIS KAGAME SASA KAGAME ABAKI YATIMA.
SOURCE Gazeti la Rai.
Rais wa Rwanda Paul Kagame aliyekuwa na uhusiano wa karibu na mwanamipango aliyemwezesha kushika dola ya nchi hiyo, Bwana Yoeri Mseni Rais waUganda, wameingia katika uhusiano hasi baada ya Rais mseven kumpa ushauri kama aliopewa na Rais Kikwete wa kuongea na waasi.
Rais Mseven aliamua kumpigia simu Rafiki yake na mdogo wake huyo kwa takribani dakika 15, akimwambia suluhu ya kumaliza mzozo wa mambo hayo ni kukaa meza moja na waasi kama alivyowahi kushauriwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania.
Rais Mseven alichukua hatua hiyo baada ya kurejea kutoka mkutano wa wakuu wa nchi za afrika za ukanda wa Afrika wa baraza la usalama kujadili masuala hayo, ambapo Rais Kagame hakuhudhuria bali aliwakilishwa na waziri wake wa mambo ya nje,
''Nakwambia ndugu yangu viongozi wote wameamua na kusisitiza ufanye mazungumzo na waasi hao maana wanaamini njia itakayofanikisha mapatano ni mazungumzo tu na hata mimi nasisitiza ufanye hivyo''
Baada ya kupokea ushauri huo wenye msisitizo, Rais Kagame aliwaita washauri na kuwaeleza hatua ya Mseveni kuwaacha peke yao.
''Nimekuwa nikiwaambia kuwa tuko peke yetu, sasa muone hata huyu ndugu wa damu kabisa aliyekuwa akitupa msimamo na kutuunga mkono nae ananipa ushauri kama wa kikwete, kuwa nikae na wauaji, hapana siwezi kukaa na wauaji kabisa tena hapana''
kisha Rais Kagame aliwaagiza watawanyike kisha kila mmoja aje na ushauri juu ya nini cha kufanya.
Rais kikwete alimpa ushauri kama huo Rais Kagame wakiwa kwenye baraza la Usalama la nchi za kusini mwa Afrika, ushauri huo wa Rais kikwete ulisababisha Rais Kagame akasirike na kujibukwa kejeli na kebehi na dharau sana, sasa hali ya kageme haina amani baada ya kubaina hata Mseveni nae aliyemtegemea hayuko pamoja ane.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments :
Post a Comment