Monday, November 18, 2013

DAVID KAFULILA : RAIS AJAYE 2015 SIO LAZMA ATOKE KIGOMA.

 BONGOAFRIKA inamshukuru sana Mh. DAVID KAFULILA kwa kujitokeza na kupangua maneno yaliyotengenzwana watunzi wa HEKAYA FEKI, kwanza niseme nilipoona hii post JF nilishangaaa sana na kuitafakari hata kama ni kweli una feeling hizo kwa ninavyokujua usingeweza kutamka hadharani hvi, lakini nikaiona hii inarudiwa tena na tena na kwa bahati mbaya sikufanikiwa kukusikia ukikanusha, juzi nilipoiona tena JF nikaamua kuileta hapa ili angalau tusikie labda utatokea hadharani kuisemea kwa kuikazia au kuikanusha ....ASANTE KWA KUMALIZA UTATA HUU..NAOMBA NIIFUTE SASA

MSOME HAPO CHINI ........
David Kafulila
Kufuatai kutapakaa mitandaoni kwa kauli zilizoanzia katika mtandao wa JF na baadae kusambaa kwenye mitandao mingine ya kijamii,
Zilizowekwa kana kwamba zinamnukuu Mbunge wa kigoma kusini David Kafulila akisema kuwa Rais 2015 lazima atokee kigoma, zikiwananga wabunge waliosimamamajukwaani kule kigoma na kutoa kauli za msisitioz juu ya kumuunga mkono rais atakaegombea Urais 2015 akitokea kigoma.
Wabunge hao walizikana kauli zao baada ya kurejea tokea safari ile waliyoifurahia na kuserebuka majukwaani pamoja na wabunge wa kigoma katika tamasha lililoandaliwa na wabunge hao.
Habari hiyo ilitoa maelezo ambayo ukiyasoma vyema utagundua kuwa yamepikwa kama kawaida ya wapikaji wasio na umakini, kauli nyingi katkati ya tamko feki zimekaa kihekaya zaidi ya kifact
Mbunge huyo wa Kigoma kusini David Kafulila (NCCR- Mageuzi) ameibuka na kusema kuwa watu wanaofanya hivyo wana lao jambo na kama kawaida yao wakiiishiwa hoja za kuruka nazo katika vijiwe vyao vya siasa za kutembelea nyota za watu watazusha lolote tu juu ya mtu ili wapate cha kunywea kahawa.

  Akiongea na BONGO AFRIKA AMESEMA......
 ''Wandugu haya ni matumizi MABAYA ya social media.
Sijawahi kusema Mimi kwamba rais ajaye lazma atoke Kigoma .
Siasa za urais na makundi ya urais upinzani na ccm nazichukia sana. 
Sasa kuna watu wanataka kulazimisha tu niseme wanavotaka wao au ambavyo wangependa kusikia kwa lengo la kushusha heshima yangu, sikupenda, haya maneno yaliwekwa Mara ya kwanza kwenye mtandao wa jamiiforums.
Nilihuzunika sana, sijui aloweka kwani wengi wanatumia majina bandia.
Niliwasiliana na mmiliki wa mtandao huo baadae kutaka kujua kwanini wanaruhusu posts ambazo hazina source?
Badae alikiri na tangu hapo kwenye aliweka ujumbe jf kuwa mtu yeyote mwenye tatizo awasiliane nae na akaweka email yake pale.
Niwambie wazi watanzania Kafulila mnaemsikia sio mwanasiasa mpuuuzi wa kusema maneno ya kijinga kiwango hicho.
JF huwa nasoma tu, naweza kuchangia labda kwa mwaka Mara mbili kwasababu sipendi namna baadhi ya wachangiaji wanavotumia kejeli, matusi, wapo wachangiaji wakiandika napenda kusoma lakin sipendi kuchangia.''

Aliendelea kusema.......
 ''Nimeamka asbh nakuta link inayosema Mimi David Kafulila Nilisema rais ajaye lazma atoke Kigoma. 
Story hii ilipata kuandikwa na mtu mmoja kwenye mtandao wa jamiiforums , bahati mbaya aliandika bila source.
 Yani alizuka tu na kuandika maneno ambayo Angetamani yaonekane Mimi nimesema, bahati mbaya alitumia jina bandia. 
Niliwasiliana na mmiliki wa mtandao huo, na akanielewa kuwa ile story ilikua na lengo lake. 
Sijawahi na singowahi kusema ujinga wa kiwango hicho. Nachukia sana mijadala ya urais inavokwenda nchi hii.
 Nashukuru mmiliki wa jamiiforums alinielewa na kutoa.
 Mimi jamiiforums huwa nikichangia labda Mara mbili kwa mwaka, lakin sipendi kuchangia kabisa. 
Huwa napita kusoma tu kwani kuna baadhi ya watu napenda kusoma maandiko Yao.mtu aloweka maneno yale alikuwa na malengo yake kwasababu zake hasa ili kunivunjia heshima niomekane nafikiri kidogo.
Tusijadili rais atoke wapi wala awe nani, tujadili issues ambazo zinahitaji kushughulikiwa ndipo tuone nani ataweza sio kwa misingi ya eneo, dini,Kabila wala rangi Bali uzalendo na uwezo wake''.

No comments :

Post a Comment

 
Copyright © 2013. BongoAfrica - All Rights Reserved.